Mbwana Samatta Na Ndoto Yake Ya Kumiliki Private Jet

Msakata kabumbu maarufu nchini Mbwana Samatta ambaye kwa sasa anacheza soka la kulipwa katika timu ya KRC Genk kutoka nchini Ubelgiji ameiweka wazi ndoto yake ya kumiliki private jet.

Samatta ambaye pia anaichezea timu ya Taifa ya Tanzania ya Taifa Stars amesema hayo baada ya kuonekekana akiwa amepiga picha mbele ya private jet ya timu yake ya KRC Genk.

download latest music    

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mbwana Samatta ameandika maneno haya kuhusiana na ndoto hiyo:

Ndoto za kumiliki private jet zimeanza baada ya kupiga picha hii, sio kila ndoto inaweza kutimia lakini wacha vita ianze”.

Samatta anafanya vizuri sana katika klabu yake hiyo baada ya kung’ara katika michezo ya kufuzu kucheza UEFA europa League,baada ya kuisadia klabu yake hiyo kufuzu katika michuano hiyo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.