MC Pilipili Ajibu tuhuma za kuiba mwanamke kwa kutumia pesa

Mchekeshaji maarufu bongo, Emmanuel Mathias ‘MC Pilipili’ ambaye hivi karibuni amemvisha pete ya uchumba, mchumba wake, amefunguka juu ya tuhuma zinazodaiwa kuwa ametumia pesa kumpata mwanamke huyo kutoka kwa mwanaume wake wa zamani.

Akiwa kwenye Mahojiano alichukua nafasi kujibu tuhuma hizo kwa kusema kuwa “Aisee nampa pole, Tanzania inaonesha wanawake ni wengi kuliko wanaume, kwa hiyo sio rahisi kwa yeye kutembea na mwanaume mwingine, lakini ni rahisi kupata mwanamke, atapata mwanamke mwingine, kwani wanawake ni wengi Tanzania na duniani”

download latest music    

Itakumbukwa hivi karibuni Mc pilipili alimvisha pete mchumba wake huyo na kuangusha kilio mbele za waliokusanyika kushuhudia tukio hilo huku baadhi ya watu kwenye mitandao wakitafsiri tukio hilo kama ni udhaifu kwa mtoto wa kiume kulia.
TOA MAONI YAKO HAPA

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.