Mh.Nape akanusha kushindwa kuwapatanisha Diamond na Alikiba

Aliyekuwa waziri wa habari na michezo ambae pia ni mbunge wa Mtama kupitia chama cha CCM mh.Nape Nnauye amefunguka kuhusu jitihaada zake za kutaka kuwapatanisha wasanii wakubwa nchini Diamond na Alikiba kipindi cha uongozi wake katika sekta hiyo ya michezo,mh. nnauye anasema kuwa sio kweli kuwa alishindwa kuwapatanisha ila jitihada hizo zilikwama kutokana na uongozi wake kukoma ghafla, kwa sababu ambayo iko wazi.

Mh.nape alipokuwa waziri wa habari na michezo alikuwa ameunda kamati iliyowashirikisha wasanii hao ili kuchangia vijana wa mpira wa miguu,kamati iyo ilikuwa na lengo la  kuwakutanisha diamond pamoja na alikiba pamoja ili kufanya kampeni za kuhamasisha wananchi kuchangia kusaidia timu ya Taifa ya Serengeti boys under 17 ambao walikuwa wanaenda kucheza nje ya nchi,Mh. nape anasema kuwa lengo kubwa  ilikuwa ni kuweka historia ya kuwafanya Diamond na alikiba kuwa na wimbo ulioimbwa pamoja hata kama hawatakutana sehemu moja yaan katika wimbo huo kila mtu awe na verse yake katiaka wimbo huo,katika kuwaunganisha huko walishatengeneza na beat ,ilikuwa ni  swala la muda wa kuwakutanisha tu ili kutengeneza wimbo.

download latest music    

Kiongozi huyo anasema kuwa bifu la Diamond na alikiba ni zuri endapo msuguano wao utakuwa mzuri kama utakuwa na manufaa ya kukuza muziki nchini  , kama mmoja anatoa wimbo huu na mwingine akatoa huu ni vizuri pia kama ilivyo sasa mmoja ametoa seduce me mwingine katoa zilipendwa, anaongezea kwa kutoa mfano wa uwepo wa wasanii wa zamani wa taarabu kama khadija kopa na Nasma Kidogo  ambao  walikuwa wanapigana vijembe lakini walikuwa wananogesha sana muziki wa taarabu kutokana na ushindani wao katika muziki huo .

Mh. Nape  alifananisha bifu la diamond na alikiba kama  ushindani wa simba na yanga ‘leo ukitaka mpira ufe basi ua bifu la simba na yanga  , ukishaliua tu na mpira unakufa ,  hivyo ndio burudani ilivyo ‘ anaongezea kuwa kama  bifu liwepo ila tu lisivuke mipaka ya kujenga chuki na kutaka kuumizana.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.