Mh.Temba Asema Sababu Za Kuvunjika Kwa Ya Moto Band

Imekuwa ni kama desturi kwa baadhi ya makundi mengi ya muziki kuvunjika na kushindwa kuendelea kufanya kazi pamoja, ilhali wanakuwa tayari walishateka soko la muziki na mioyo ya mashabiki wa muziki, ndicho kilichotokea kwa kundi la muziki wa Ya Moto Band , kundi lililokuwa likifanya vizuri na kupendwa na watu wengi katika muziki wao waliokuwa wanaufanya,lakini pia umaarufu wao haukuwa tu nchini Tanzania bali hata nje ya nchi, .Kwa sasa kundi ilo la muziki limevunjika huku kila msanii akitafuta ustaarabu wake wa kufanya kazi zake za kimuziki, inaweza kuwa bahati nzuri au kipaji cha msanii ndicho kinaweza kumpelekea kuendelea kufanya vizuri katika muziki kwa upande wao.

Sababu za kuvunjika zimekuwa nyingi lakini hakuna anaekuja na jibu kamili kuhusu kuvunjika kwa kundi ilo , Mh. Temba ameibuka na kuongelea sababu za kuvunjika kwa kundi ilo, akiwa kama mmoja wa waanzilishi na mlezi wa kundi ilo la muziki tangu wakiwa chini mpaka wameanza kujulikana Mh. Temba anaasema kuwa shida kubwa ya kuvunjika kwa kundi ilo ni kuvamiwa na watu wenye ela.

download latest music    

Akiongea na East Africa  katika kipindi cha Planet Bongo, Mh.Temba anakiri kuwa kundi ilo lilianza kuingiliwa kati na watu wenye fedha na kutaka kuwamiliki wasanii bila kuangalia wasanii hao wametoka wapi huko nyuma.”mimi nakupa mfano wa hawa Ya moto band,utaona labda mtu anasimamia msanii fulani,,mbona hakumchukua mwanzoni wakati  hajulikani, kabla hatujamkuza na kuwa superstar” alifunguka Mh.Temba

kwa maoni yake anasema kuwa kama hao wenye pesa walitaka kusaidia wasanii basi wanapaswa kutafuta vipaji vipya mitaani viko vingi na wanaitaji kuinuliwa lakini sio kuja kuingilia kwa wasanii ambao tayari walishakuzwa na wana majina tayari’huyo mtu kama anauwezo  kwanini asingekuwa na vipaji vyake,wewe unaona nuru tayari inangaa ndo  unaenda kuchomoa pale” aliongezea Mh. Temba

undi la Ya Moto Band lilikuwa likiundwa na Aslay, Enock Bella, Maromboso na  Beka Flavour, lakini kwa sasa kundi ilo kila mmoja anafanya kazi kwa kujitengemea huku Aslay akiwa  chini ya menejimenti ya Chambuso . Hata hivyo baaada ya kundi ilo kuvunjika msanii anaeonekana kufanya vizuri kuliko wote  ni Aslay huku wengine wakioneka kushindwa kabisa kutokana na ukimya wao.kundi ili kuvunjika na dalili mbaya ya kupotea kwa vipaji vya muziki.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.