“Mimi naibiwa haki yangu vipi?” Matonya adai wimbo mpya ya Diamond umeibwa kutoka kwake

Diamond na wasanii wote wa Wasafi waliachia wimbo mpya ‘Zilipendwa’ Ijumaa Agosti 25. Wimbo huo umezua utata kwani msanii Matonya anadai kuwa wimbo huo uliibwa kutoka kwake.

Matonya alitoa malalamiko yake kwenye mtandao wa Instagram ambapo alidai kuwa ana haki zake katika jina hilo la ‘Zilipendwa’. Staa huyo aliwai toa ngoma la jina hilo hilo zamani.

download latest music    

“Nduguzangu wasafi / Nawapongeza sana kwa kazi mzuri mnazo zifanya / Nilifurahi Sana mlichokifanya kwa saida karoli dadaetu/ mlimuita mkamshirikisha akawapa Baraka zake/ kwangu mlishindwa nini? Sina shida Ya Pesa nina shida Ya heshima cose najua dunia ni mapito/ kama mimi naibiwa haki yangu vipi wasanii wachanga? Basata mkowapi? Wadau Wa muziki mkowapi? Usipo ziba ufa tajenga kuta!! Khaaa tena Bila woga???? lakini haki itafata mkondo wake,” Matonya aliandika.

Tazama wimbo huo hapo chini:

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere