Mimi Naimba Hip hop hata Kama Wakikataa- Nay wa Mitego

Mwanamuziki wa Bongo Fleva Nay wa Mitego ameibuka na kujitamba kua yeye ni mwanamuziki wa Hip hop na kuwa anapendwa sana na mashabiki kwa ajili ya staili yake ya kipekee ya kurap ambayo iko tofauti na wasanii wengine.

Nay aliyasema hayo kwenye mahojiano aliyoyafanya kwenye kituo kimoja cha redio ambapo alisema kuwa kuna baadhi ya wasanii wenzake wa hip hop wamekuwa wakidai haimbi hip hop lakini amesema huo wote ni wivu kutoka kwa wasanii hao kutokana na mafanikio anayoyapata kuwashinda wenzake.

download latest music    

Nay amedai kuwa kama kweli angekuwa haimbi hip hop basi asingepata mashabiki wengi na kupendwa kuliko hao wasanii wengine wanavyopendwa. Ny ambaye anasifika kwa staili ya ya kuimba na kusema ukweli juu ya mambo mbalimbali hasa siasa au hata kuongelea wasanii wenzake na kazi zao.

Nay ambaye kwa sasa natamba na nyimbo yake mpya inayoenda kwa jina la ‘Makuzi’ ambayo amefanya kwa staili ya kuimba ambayo huenda ndio sababu wasanii wenzake wamemtoa kwenye kundi la kurap kwani nyimbo yake nyingine ya ‘Acheze’ imeimbwa pia lakini ngoma kama ‘Wapo’ na ‘Moto’ alizotoa mwaka huu aefanya kwa staili ya kurap.

Hata hivyo Nay amedai kuwa wasanii wenzake hao wakisema haimbi hip hop hakumuumizi kwani yeye anaangalia maslahi na kama anachofanya kinamuingizia kipato basi haina shida wasanii wenzake waseme nini kwani muziki kwake ni biashara.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.