Mimi Sina Competition na Shiloleh:-Esha Buheti

Mwanadada wa bongo movie esha buheti amefunguka na kuongelea uhusiano wake na shiloleh kama watu ambavyo wamekuwa wakiwashindanisha katika swala zima la mapisha na kusemekana wawili hao kwa sasa hawaelewani kwa sababu hiyo,

Akiongea na mwandishi wa habari, esga anasema kuwa kwa upande wake hana ushindani na mtu yoyote zaidi ya kwamba anachojua kila mtu anafanya kazi zake mwenyewe na kila mtu ana wateja wake lakini pia anshangaa kwanini watu wengi wamekuwa wakimshindanisha na yeye wakati kuna wasanii wengi tu ambao ni wapishi.

download latest music    

Competion gani, mimi si-compet na mtu yoyote na hakuna biashara mamabyo ni ya mtu  au kuwa hii imepangwa kufanywa na mtu fulani tu hapana,na hayo ni maneno ya watu nimekuwa nikiyachukia sana kwa sababu mimi sina competition na shiloleh , kwanini mbona watu wengi wanapika tu kuna open kitchen anapika , uwoya anapika lakini wao wamekazana na shiloleh tu kuna nini au vigezo gani vya kunilinganisha nae.

Siwezi kulinganishwa na shilole kwa sababu yeye nilishamkuta akifanya alafu hata menu zetu ni tofauti sana.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.