Mipango ya ndoa ya Shilole sasa imeiva

Zuwena Mohammed maarufu kama Shilole sasa yuko tayari kuwa mke wa mtu. Mrembo huyo sasa amebaki na miezi mbili tu afunge ndoa na mpenzi wake.

Kitu ambacho kimebaki kwa sasa ni kutoa kadi za mwaliko kwa ndugu, jamaa na marafiki kwani Shilole atafunga ndoa Oktoba, mwaka huu, jijini Dar es Salaam.

download latest music    
Shilole

Msanii huyo aliambia Mtanzania kuwa anamshukuru Mungu na amewataka wasanii wenzake na mashabiki kumpa sapoti katika ndoa yake.

“Mipango ya ndoa inakwenda vizuri, hivyo Oktoba mwaka huu utakuwa mwezi wetu ambao Mwenyezi Mungu atatubariki kuunganisha familia,” alisema Shilole.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere