Miriam Odemba Akiri Kutamani Kuzaa na Diamond

Mwanamitindo na mlimbwende Miriam Odemba anefunguka na kuanika mapenzi yake kwa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz na kukiri kuwa anatamani kumzalia Mtoto wa nne.

Ijumaa Wikienda linaripoti kuwa Miriam Odemba alifunguka hayo kwenye mahojiano waliyofanya naye kwa njia ya simu kutokea nchini Ufaransa anapoishi sasa.

download latest music    

Kwenye mahojiano hayo Miriam alijikuta akimfungukia Diamond kwa kusema amekuwa akiangalia mwenendo wake na kumuona ni ‘baba bora’ hivyo si vibaya akimzalia mtoto mmoja.

Odemba alisema anafuatilia watoto wa Diamond, wale wawili aliozaa na mwanamama mjasiriamali wa Kiganda, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ na yule wa mwanamitindo Hamisa Mobeto na kugundua anawalea vizuri, kitu ambacho kinamshawishi na yeye awe tayari ‘kumtunuku’.

Diamond nampendaga pia anavyojua kuangalia watoto wake mpaka kuna wakati natamani mimi ningezaa naye mtoto mmoja pia ni  kijana mdogo, lakini anaweza kujali familia yake na watoto wake japokuwa hayupo vizuri na mama wa watoto hao (Zari na Mobeto), hapo ndipo anaponikosha sana”.

Alipoambiwa afafanue kwa njia gani anaona Diamond anawajali watoto wake, Diamond alifunguka:

Unajua mara nyingi naweza kumuona anatoka Tanzania na kwenda Sauz (Afrika Kusini), kwa ajili ya kuona watoto wake japokuwa hayuko tena kwenye mapenzi na mzazi mwenzake”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.