Miss Tanzania Afungukia Tetesi Za Bifu na Basila

Mashindano wa shindano la Miss Tanzania mwaka 2018/2019 Queen Elizabeth Makune amefungukia tetesi zinazosambaa kuwa huenda ana Bifu na Basila Mwanukuzi.

Queen Elizabeth anatajwa kuwa na Bifu na Mratibu wa shindano la Miss Tanzania Basila Mwanukuzi kisa kikitajwa na kamati yake kushindwa kupewa zawadi alizoshinda kwenye shindano hilo mwaka jana.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Mchanganyiko, Queen Elizabeth alisema, hana ugomvi wowote na Basila na maneno yanayoongelewa na watu yana lengo la kutaka  kuwagombanisha.

Ningeomba niweke wazi kuwa sina matatizo yoyote na mratibu wa shindano langu, Basila Mwanukuzi, tena ninampenda sana, nipo naye vizuri tu, ningependa maneno yanayoongelewa na watu yapuuzwe, tuangalie mambo ya maendeleo ili tuweze kufika mbali zaidi na kuitangaza nchi yetu”.

Queen Elizabeth aliiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss World mwaka jana Lakini alishindwa kufanya vizuri na moja ya sababu zilizotajwa ni maandalizi mabovu kutoka kwa kamati

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.