Miziki ya Ali Kiba na Mwana FA Yatambulika Kimataifa Zaidi

Wanamuziki Ali Kiba na Mwana FA wamekula shavu zito baada miziki yao wanayofanya kutambulika na wasanii wakubwa wa Marekani.

Mwanamuziki Ali Kiba ambaye kwa sasa anatamba na wimbo wake wa ‘Seduce me’ ameula kwani wimbo wake huo umekuwa miongon ati ya nyimbo zilizochezwa na DJ katika uzinduzi wa wa bidhaa za mbalimbali za BallyxSwizz zinazomilikiwa na mwanamuziki na producer mkubwa Marekani Swizzbeats ambaye pia ni mumu wa mwanamuziki mkubwa duniani Alicia Keys.

download latest music    

Model wa kimataifa toka Tanzania Flaviana Matata ambaye alikuwa mmoja wa wahudhuriaji katika sherehe hiyo alituma clip ya video katika mtandao wake wa twitter na kuandika

“When you go to support a friend and his DJ plays Tanzanian music Swiss Beats thanks for support”.

Pia katika sherehe hiyo model Flaviana Matata alikutana na Mwanamuziki maarufu anayeenda kwa jina la ‘Fabolous’ ambaye alitaja mistari ya ‘Unanijua unanisikia’ ambayo inapatikana katika nyimbo ya Mwana FA inayoitwa Unanijua unanisika katika hali ya kuonyesha furaha yake na shukrani Mwana FA aliyumia mtandao wa twitter kumshukuru rapper huyo na model huyo kwa kumfikishia ujumbe huo.

Hiyo yote inaonesha ni kwa jinsi gani muziki haujalishi lugha inayotumika kwani Faboulous hajui kiswahili lakini ametokea kuvutiwa na wimbo huo pamoja na kutokujua maana ya wimbo huo pia ni vizuri kuona lugha yetu inakua zaidi.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.