Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam atoa onyo kwa Alikiba na Diamond

Mhe Paul Makonda, Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, ametoa onyo kwa Diamond Platnumz na Alikiba kuhusu kushindana kwao kimuziki.

Makonda alikiri kuwa ushindani wa kimuziki baina ya Diamond na Alikiba unachangia kukuza muziki wa Bongo lakini hata hivyo alionya kuwa lazima wasanii hao wazingatie sheria na maadili ya jamii wanaposhindana.

download latest music    
Mhe Paul Makonda

“Tofauti zenu mimi nazipenda, kwani zinaleta ushindani mzuri kwenye mziki. Ila naomba mzingatie sheria na Utamaduni wetu..,” Paul Makonda aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Alikiba na Diamond waliachia nyimbo zao mpya ‘Zilipendwa’ na ‘Seduce Me’ siku moja, Ijumaa Agosti 25. Tazama nyimbo hizo hapo chini:

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere