“Mnaochonga Kuhusu Ndoa Yangu Hayawahusu”-Ben Kinyaiya

Mtangazaji wa Channel Ten na muigizaji wa Tamthilia ya Huba, Ben Kinyaiya ameibuka na kuwatolea Povu zito watu wanaoendelea kuichokonoa ndoa yake.

Jumamosi iliyopita  Ben  alifunga ndoa ya kiserikali na mwanamke wake huyo ambaye anatajwa kuwa mchumba wake wa siku nyingi, baada ya picha zao kusambaa katika mitandao ya kijamii.

download latest music    
Ben Kinyaiya na Mpenzi Wake

Mara baada ya picha hizo za harusi kusambaa, mara moja maneno yaliibuka kutokana na muonekano wa bibi harusi ambapo wapo waliodai kuwa mwanamke huyo ni mtu mzima kuliko Ben ‘Shuga Mama’.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Jumamosi, Ben amewajia juu watu ambao wanaiponda ndoa yake na kuwataka waache kumfuatilia kwani huo ni uamuzi wake binafsi na wala hakulazimishwa na mtu.

Wale ambao wananisema kuhusu ndoa yangu hayawahusu, maana wanaongea sana. Wapo wanaosema mara nimefuata pesa, mara ni kwa sababu nataka kwenda kuishi Uingereza, mimi hayo siyaelewi kwa kuwa wao ndiyo wanayaongea.

Mimi ninasisitiza tu kuwa wanaweza kuzungumza mambo mengi, lakini ukweli ni kwamba hayawahusu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.