Mobetto Hawezi Kuwa Tanzania Sweetheart ni Wema Peke Yake-Maimartha Jesse

Mtangazaji maarufu na mfanyabiashara Maimartha Jesse ameibuka na kumkingia kifua Msanii wa Bongo movie Wema Sepetu na kudai hakuna kama yeye.

Siku za hivi karibuni Kumekuwa na mjadala Kwenye mitandao ya kijamii ambapo Hamisa Mobetto amekuwa akipambanishwa na Wema Sepetu na watu hata kusema title ya Wema ya Tanzania Sweetheart anatakiwa apewe Mobetto kwani ndio anapendwa kuliko Wema.

download latest music    

Katika interview aliyofanya na Global Publishers, Maimartha amesema hakuna na hatatokea mrembo mwingine anayependwa na kukubalika kama Wema hivyo wanaompigia debe Mobeto kwamba ndiye anayekubalika sana kwa sasa wanajisumbua tu.

Wema ndiye Tanzania Sweetheart, hakuna wa kufanana naye na hatatokea mwingine kama yeye, hii ni namba nyingine, wanaosema Mobeto anamzidi ni waongo na hawajafanya tathmini zao vizuri, Wema anapendwa na kila mtu kuanzia watoto hadi wazee“.

Pamoja na kutokea kupingwa na kuchukiwa na mashabiki siku za hivi karibuni mpaka kutakiwa kuacha kujiita Tanzania Sweetheart Mrembo Wema Sepetu amegoma kuachia jina hilo na kusisitiza yeye ndio Sweetheart wa East Africa nzima.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.