Mose Iyobo Afungukia Tetesi Za Kuondoka WCB

Dansa maarufu kutoka WCB ambaye ameshaonekana kwenye video na show mbali mbali  za Diamond Platnumz, Mose Iyobo amefungukia tetesi za kuhama.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Mose Iyobo amesema hayo maneno hata yeye ameyasikia lakini hayana ukweli wowote na yote yamezuka kwasababu ya kutoonekana katika video ya Tetema ya Diamond na Rayvanny.

download latest music    

Iyobo amesema kuwa hakuonekana kwa sababu ratiba ziliingiliana kwani siku waliyokuwa wanashuti yeye kuna kazi zake alikuwa anafanya.

Kwanini niondoke WCB? Yaani kutokuwepo kwenye video ya Tetema tu basi ishakuwa nongwa? Mimi ni WCB damu yaani sio wa kuondoka leo wala kesho na sijawahi kuwaza.

Sababu ya mimi kutowepo kwenye video ni kutokana na ratiba ambazo ziliingiliana ndio maana sikuwepo lakini sio kwamba najitenga ama nataka kujitoa hapana kwakweli hizo habari ni za uongo”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.