Mr.blue Hana Beef na Diamond Platinumz.

Msanii wa  muziki nguli Bongo Mr.Blue amefunguka na kukanusha maneno yanayosambaa katika mitandoa kwa muda mrefu  ya kusema kuwa yeye na msanii mwenzie wa muziki Diamond Platinumz wako katika beef zito linalowafanya washindwe kufanya kazi za muziki kwa pamoja.

Mr.Blue amesema kuwa yeye na Diamond walishawahi kufanya kazi mbili  hapo nyuma labda kwa sasa wafanye tena lakini sio kweli kuwa  yeye na Diamond wana beef linalowafanya washindwe kushirikiana.mMr blue anasema kuwa kwa sababu watu wamekuwa wakizusha kuhusu beef lao basi kama kuna uwezekano watafanya kolabo tena ili kuthibitisha kuwa hakuna beef kati yao.hata hivyo anasem akuwa kitu kikubwa kinachowafanya washindwe kufanya kolabo ni kwa sababu wote ni wasani wakubwa na kunakuwa na u-busy kati yao wa kushindwa kukutana.

download latest music    

ni mtu nilishashirikiana nae  sio kitu cha kushangaza kwamba  labda kusema haitawezekana kufanya nae kazi pamoja,lakini unajua shida mnapokuwa wasanii wakubwa kila mtu anakuwa busy  kwa upande wake lakini ikija kufanyika kolabo kati yangu na yake basi inakuwa kitu kizuri sana kwa sababu tutawaonyesha raia kuwa hatuna beef lolote.

kwa kwelie sina tatizo lolote na diamond , ni mdogo wangu ninamuheshimu na ninaheshimu hustle zake, na amekuwa mfano wa kuigwa kwa watu.hayo mambo mengine tusiyachukulie sana serious.

Diamond na Mr blue walishawahi kufanya kazi kwa pamoja kama katika  nyimbo ya BBM  ambao waliimba wakiwa na msanii mwenzao ambae sasa hivi ni marehemu , Ngwea.na pia wimbo wa Dimaond  ambao unajulikana kama kiss to the lady .

Wasanii wengi wanakuwa na beef na migogoro isiyokuwa na maana inayowafanya washindwe kufanya kazi pamoja na kukuza soko la muziki, Mr.Blue anasisitiza kuondoa tofauti zinazotokea kati ya wasanii ili kukuza muziki wa Tanzania.

kwa upande wa diamond kumekuwa na tetesi nyingi za yeye na wasanii wengi kutokuwa na maelewano mazuri ambapo wasanii kama bob junior, alikiba ambao wamekuwa wakishindwa kukaa meza moja na kuzungumza yakaisha na kurudi kufanya kazi pamoja.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.