Mrembo Irene Amekiri Kuwa Alibeba Ujauzito Wa Diamond (video)

Mrembo na Video queen maarufu Irene au maarufu mitandaoni kama Officiallynn amefunguka na kukiri kuwa miezi michache iliyopita alibeba ujauzito wa Diamond lakini kwa bahati mbaya ujauzito uliharibika.

Irene  alijipatia umaarufu zaidi baada ya kutokea kwenye video ya msanii wa Wasafi Classic Co. (WCB) anayejulikana kama Rayvanny kwenye wimbo wake wa kwetu na natafuta kiki.

download latest music    

Lakini Irene alizidi kujipatia umaarufu pale habari zilipoanza kusambaa kuwa anatembea na msanii maarufu wa Bongo fleva, Diamond Platnumz lakini taarifa hizi zilipata umaarufu zaidi kwa sababu katika kipindi hiki chote Diamond bado alikuwa jwenye uhusiano na mama watoto wake Zari.

Habari za Irene kuwa na mimba ya Diamond zilianza kusikika miezi michache iliyopita lakini kulikuwa hamna uhakika wowote kuwa kama taarifa hizi zina ukweli wowote kwani kuna watu waliodai kuwa mimba ile ilikuwa ya msanii Rayvanny, lakini tetesi hizo zilisimama baada ya mimba hiyo kuacha kuonekana na watu kudhani kuwa ameitoa au alikuwa hana mimba kabisa.

Siku ya Jana Irene alifanya mahojiano na Dizzim Online na katika mahojiano hayo Irene alikiri kuwa ni kweli alikuwa mjamzito na Mimba hiyo iliharibika na baba alikuwa Diamond:

Nilikuwa nina Mimba kweli ila ikaharibika, na ilikuwa ya Diamond”.

Tetesi za Diamond kutoka na mrembo Irene zilizidi kushika hatamu hata pale ishu ya Hamisa ilipobumburuka kwani kuna taarifa mbali mbali zilizoenea mtandaoni kuwa walionekana nchini South Africa pamoja.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.