Msami Amefungukia Bifu Lake na Irene Uwoya

Dancer na msanii maarufu Msami Baby amefunguka na kuongelea sakata linaloendelea kutengeneza headlines hivi sasa kati yake na staa wa Bongo movie Irene Uwoya.

Msami na Irene Uwoya walishawahi kuwa Kwenye Mahusiano ya kimapenzi miaka ya nyuma lakini walikuja kuachana na Uwoya amemshirikisha kufunga ndoa na staa wa Bongo fleva Dogo Janja.

download latest music    

Uwoya na Msami walirudi kwenye headlines za mitandao ya kijamii siku ya juzi baada ya Uwoya kuposti maneno yenye utata na kisha Msami naye kumjibu kwa kejeli kuhusu ndoa yake jambo lililozua maneno na watu kufikiri labda wana bifu.

Msami ameongelea suala hilo Kwenye Interview aliyofanya na Soudy Brown kwenye You heard ya XXL:

Mbona mimi sijaona kibaya pale alichoposti Irene mimi naona kama kanisifia kuwa The best dancer in Africa ? Mbona mimi naona kama hajanipaka yaani hajanidhihaki”.

Msami amesema hajui kuhusu ndoa yake hata kama ameolewa lakini hajawahi kumwambia kuwa ameolewa na hata wakikutana hawaongei kuhusu ndoa yake na kuhusu kumposti amesema labda Irene anamiss maudambwi dambwi yake.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.