Msanii Kutoka Kenya Atangaza Nia Ya Kumuoa Zari

Mwanamuziki wa nyimbo za Injili kutoka Kenya anayejulikana kama Ringtoneapoko amefunguka na kudai yupo tayari Kuwa na Zari baada ya kutangaza kuachana na Diamond.

Wiki iliyopita siku ya Wapendanao Zari alitangaza kuwa ameamua kumuacha Baba watoto wake na mpenzi wake Diamond huku akisisitiza kilichompelekea kufikia uamuzi huo ni Diamond kuzidisha michepuko.

download latest music    

Baada ya tukio hilo Kumekuwa na maneno mengi yamekuwa yanasemwa huku linalowatatiza wengi ni kama kweli wawili hao wameachana kwani Kumekuwa na maneno mengi yanasemwa huku ikidaiwa wawili hao wanatafuata kiki na hawajaachana jambo ambalo Zari amelikataa.

Huku drama ya Diamond na Zari ikiwa inaendelea msanii Ringtoneapoko kutoka Kenya amejitokeza na kusema anataka kumuoa Zari huku akidai amesikitishwa na kitendo ambacho Zari amefanyiwa na Diamond.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ringtoneapoko aliandika ujumbe huu kwa Zari:

Leo tumenunua ng’ombe 42 ambazo tumepanga kupeleka Uganda kwa waking Zari wakati ukifika. Na kieleweke vyema kama mwanaume hajalipa mahari huyo msichana bado sio wake. Ama namna gani???? Na please mwambieni Diamond asimtolee Zari wimbo aende atoe mahari kama all serious. For us tupo tayari kwenda Uganda na tulipe hatuogopi tunafunga na kumuomba Mungu atupe ushindi”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.