Msanii Kuwa na Baunsa ni Kulinda Status Yako:-Dully syskes

Msanii wa siku nyingi Dully Sykes amefunguka na kusema kuwa kuna umuhimu mkubwa kwa msanii kuwa na mlinzi wa kutembea nae kwa sababu kuna mambo mengi yanayotoka mitaani na kwa sababu za kiusalama ni bora kuwa na mtu wa kukusaidia kwa hilo.

Dully anasema kuwa sio kila mtu ana kuwa na nia nzuri na wewe hivyo ni lazimakuwa na mlinzi wa kutembea nae, kwa sababu hata yeye amekuwa na mlinzi kwa muda mrefu na amemsaidia sana kwa maswala ya ulinzi.

download latest music    

msanii kuwa na mlizni hiyo ni moja ya kulinda status yako, na pia sio kila mtu ambae unakutana nae basi  anakuwa na lengo zuri na wewe,mimi niliamua kutembea na mlinzi ili awe ananilinda  kwa sababu sio kila sehemu ni nzuri.

Wasanii wengi sana kwa sasa wameamua kuwa wanatembea na walinzi, moja wapo akiwa ni Diamond Platinum huku sababu kubwa ilikuwa ni sababu za kiulinzi.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.