Mume wa Aunt Ezekiel arejea Dar baada ya kutumikia kifungo chake Dubai

Image: Aunty Ezekiel

Aliyekuwa mume wa Aunt Ezekiel anasemekana kurujea Dar baada ya kukawia Dubai alikokuwa akitumikia kifungo chake kutokana na kuishi kinyume cha sheria huko Dubai.

Aunt Ezekiel

Habari hizi zilienezwa na Chanzo kilichodhibitisha kuwa Sunday Demonte yuko Tanzania. Hata hivyo Risasi Mchanganyiko ilizungumza na mdogo wa Demonte, ambaye alisema;

download latest music    

“Sunday mbona ameshatoka kitambo, yupo zake uraiani kwa raha zake, ni mwaka huuhuu ametoka japo sikumbuki ulikuwa mwezi wa ngapi maana sikuwepo, kwa sasa yupo hapa Dar, hayupo Dubai, ukitaka kujua mengi ni vizuri nikuunganishe naye mwenyewe ukamuhoji,” alisema.

Mose Iyobo na Aunty Ezekiel

Hata  hivyo bado wengi wanangoja kusikia atakachosema Aunt Ezekiel ambaye sasa anatoka kimapenzi na dancer wa Wasafi records, Mose Iyobo.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua