Mume wa Mama Diamond Afunguka Kuishi Madale Kwa Diamond

Mume wa Mama mzazi wa Diamond Bi. Sandra aitwaye Shamte Maisala ambaye kwa sasa ndiye baba wa kambo wa msanii Diamond Platnumz, amefungukia tuhuma za kuishi Madale.

Katika mahojiano yake na Global Publishers, Shamte amesema kuwa, anashangazwa na maneno hayo kwani ana kwake lakini anaishi Madale kwa kuwa kote ni nyumbani kwake. Amesema, kikubwa anachokitaka kutoka kwa mkewe ni heshima ya mume na anaipata hivyo suala la kuishi kwake siyo ishu.

download latest music    

Unajua watu wamekuwa wakihoji sana sababu ya mimi kumuoa mama Diamond na kuishi kwake lakini wanasahau kuwa zote ni nyumba, siku tukiamua kukaa Bunju (kwake) tutakaa na siku tukiamua kukaa Madale tutakaa kama tunavyokaa sasa, ishu si makazi bali ni heshima ya mume kwani napikiwa, nafuliwa na huduma zote napata”.

Baada ya Diamond kununua Jumba la kifahari maeneo ya Mbezi beach mapema mwaka huu aliamua kuhama Madale na kumuachia Nyumba mama yake na baba yake wa kufikia.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.