Mwana FA: Sijawai tumia vyeti vyangu vya shule kuomba mtu kazi

Watu wengi huenda shule na matarajio kuwa watatumia vyeti vyao kutafuta kazi, lakini Mwana FA hajawai tumia vyeti vyake kutafuta kazi kokote.

Staa huyo wa Bongo Fleva amefunguka na kusema yeye alienda shule kupanua ubongo wake ili aweze kumudu mazingira yake ya kila siku.

download latest music    

“Sijawahi ku-apply (kuomba kazi) kusema kweli nafikiri namna kwenda kazini saa 12 asubuhi na kutoka saa 11 inanipa wakati mgumu. Sisi tunasoma kwa ajili ya unajaribu kupanua ubongo wako ili uweze kumudu mazingira yako ya kila siku ama ukitaka kufanya kazi zako uzifanye kwa ule upeo umeupata shuleni. Sasa sisi tunasoma kwa sababu uje na vyeti uajiriwe, siyo usahihi wa watu kwenda shule, kwa hiyo mimi natumia vyeti vyangu lakini sivitumii kwenda kumfanyia kazi mtu yeyote, sivi-apply kwenye muziki, navi-apply kwenye biashara zangu nyingine,” Mwana FA alisema katika kipindi cha The Playlist cha Times FM.

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere