Mwanamuziki Quick Rocka Ampigia Saluti Diamond Platnumz

Mwanamuziki wa Bongo fleva Quick Rocka ameibuka na kumpigia saluti Diamond na kudai kuwa rekodi yake aliyoiweka ni nguma kuivunja.

Diamond alivunja rekodi hiyo baada ya wimbo wake wa Hallelujah aliyomshirikisha Morgan Heritage kufikisha jumla ya views milioni moja ndani ya masaa kumi na tano na kufikisha milioni mbili ndani ya siku moja.

download latest music    

Kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram mwanamuziki Quick Racka alituma video akimpa hongera Mwanamuziki mwenzake Diamond Platnumz na kumpongeza pia kwa video kali aliyofanya na pia kumsifia mwanamuziki Morgan Heritage aliyemshirikisha.

“Hatari mzee big shout out to Diamond Hallelujah is a dope song meen Morgan Heritage ameua we mwenyewe umeua you know what am saying so i appreciate good work brother and the video its a movie so big shout out to you one million views in fifteen hours man thats a record man ujue labda atokee mwingine avunje rekodi in twelve hours lakini rekodi hiyo ngumu sana kuvunjwa salute brother dope tune”.

Diamond alivunja rekodi iliyowekwa na Ali Kiba kupitia wimbo wake wa seduce me wiki chache zilizopita na pia  na pia Quick Rocka alimpongeza Ali Kiba kwa mafanikio yake.

Wewe umeupokeaje wimbo huo mpya wa Diamond  Je unahisi atatokea mwanamuziki wa kuvunja rekodi ya Diamond?

Tafadhali toa maoni yako.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.