Mwarabu Fighter Athibitisha Bado Yupo WCB Hajafukuzwa Kazi

Bodyguard wa staa wa Bongo fleva na CEO wa WCB, Diamond Platnumz, Mwarabu Fighter ameibuka na kuweka wazi kuwa taarifa zilizosambaa kuwa amefukuzwa kazi sio za kweli.

Wiki chache zilizopita kuna taarifa zilisambaa kuwa Mwarabu Fighter amefukuzwa kazi na kudaiwa kuwa aliambiwa na Diamond akae nyumbani mpaka pale atakapopata taarifa.

download latest music    

Kwenye Interview na Global Publishers, Mwarabu amekanusha tetesi hizo na kusema kuwa bado yupo WCB na anaendelea kufanya kazi na Diamond kama kawaida, kutokumuona naye ni kwa sababu ya taratibu za kiofisi ambazo hawezi kuziweka wazi ila siku yoyote tutamuona naye.

Taarifa za Mwarabu kufukuzwa ziliaminika kwa sababu aliokuwa anaonekana yuko Tanzania Wakati Diamond yupo na timu yake nchini Marekani kwa ajili ya Tour yake ya ‘A Boy from Tandale’.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.