Mwasiti Aamua Kumjibu Linex Kuhusu Wimbo wa Leka Dutigite

Ikiwa ni siku chache zimepita tangu msanii kutoka mkoa wa Kigoma Sunday Linex Mjeda alipofunguka na kusema kuwa asilimia kubwa ya wimbo wa lekadutigite ulitengenezwa na kutayarishwa na yeye, msanii  mwenzake kutoka Kigoma mwanadada Mwasiti Almasi amefunguka na kusema kuwa Linex kwa sasa hapaswi kuzungumzia mambo hayo zaidi ya kukaa na kuangalia jinsi gani ya kufanya kitu kikubwa kuliko  kile.

Aache kuongelea vitu vilivyopita, lekadutigite ilishapita nadhani kwa sasa inabidi tuangalie yale yaliyopo tu kama familia lazima kuangalia kitu gani tena kinaweza kutuongezea manufaa lakini sio nani kaandika mistari mingapi, au mistari mingi , maana hiyo ni zaidi ya miaka minne sasa.-Aliongea mwasiti katika XXL ya Clouds Tv

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.