“Mwenyezi Mungu Ndio Muumbaji Wa Wanyonge na Wajanja”- Ujumbe Wa Ali Kiba Kwa Ommy Dimpoz

Staa wa muziki wa Bongo fleva Ali Salehe Kiba amemtumia salamu za Birthday njema Msanii mwenzake na rafiki yake Omary Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz.

Siku ya leo ni siku ya kuzaliwa ya Ommy Dimpoz na rafiki yake na mtu wake wa karibu kabisa Ali Kiba kamuwish Birthday njema na ujumbe mzito.

download latest music    

Ali Kiba amemtaka asijali sana wala asiyawaze yale magumu aliyopitia Miezi michache iliyopita baada ya kulazwa hospitali kwa Miezi karibia mitano badala yake amshukuru tu Mwenyezi Mungu.

https://www.instagram.com/p/Bnp-7T9ll_E/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1azp61dlmsurf

Kwenye posti yake ya leo ya birthday Ommy Dimpoz amemshukuru sana Ali Kiba kwa kuwa naye kipindi chote cha ugonjwa na hata kuweka wazi kuwa amemuuguza.

Ali Kiba alisimamisha kuachia kinywaji chake  cha Mofaya Miezi michache iliyopita baada ya kukizindua kutokana na maradhi ya Ommy Dimpoz.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.