Mzee Yusuph Aombea Dua Muziki wa Taarabu Uanguke.

Msanii mkongwe wa siku nyingi Mzee Yusuph ambae alistaafu muziki na kujikita katika maswala ya din amefunguka na kusema kuwa hajui kuhusu maendeleo ya muziki huo kwa sasa lakini kama muziki huo unakufa basi kwake hana shida zaidi ya kuuombea dua ufe kabisa ili wasanii wake watafute kitu kingine cha kufanya.
Alhaji Mzee Yusuph amesema kuwa kama taarabu inayumba ataomba dua ianguke na watu watafute vitu vizuri zaidi. “Siijui na siisikilizi yaani sijapata nafasi ya kuusikiliza na sitaki kabisa kujua kunaendeleaje kama kuna yumba ntaomba dua zaidi kuanguke kusiyumbe, watafute vitu vizuri zaidi ya taarabu ,” alisema Mzee Yusuph katika mahojiano yake na Azam Tv.
Nimeacha taarabu wakati bado napenda unaelewa huyo kuacha wakati unapenda na nikamuomba Allah nikamwambia napenda hiki kitu lakini nakiacha, sasa nijaalie nikichukie maana yake nimeacha kitu ambapo bado kinaendelea kufanya maisha.”

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.