Nahrel Kuanza kazi na Akon na Kery Hilson
Nahrel ni mja ya wasanii na watayarishaji wakubwa wa nyimbo nchini na kutokana na ufanyaji kazi nzuri amekuwa akijulikana nchini, Afrika na Duniani kwa ujumla , lakini hivi karibuni Nahrel amesema kuwa kwa sasa amekuwa busy sana kiasi kwamba inabidi anaetaka kufanya nae kazi basi inabidi mtu huyo awee kumshawishi sana.
Basi ukweli ni kwamba licha ya kufanya ngoma nyingi za wasanii wakubwa barani Afrika akiwemo Mr. Eazi na Patoranking, tayari mkali huyo wa midundo ameshafanya kazi na Akon na Kery Hilson.
Akithibitisha taarifa hizo mzazi mwenzie wa kundi la Navy Kenzo, Aika amesema kuwa tayari Nahreel ameshamaliza kufanya kazi hizo na kinachosubiriwa ni muda tu.
“Kuna meneja wetu mmoja nchini Marekani ambaye amejaribu kumfanya Nahreel afanye kazi na Akon.. na Kery Hilson soo! Nahreel soon anafanya nao kazi,“amesema
Lakini pia ulikuwa hujui basi nikujuze, kuwa Nahreel ana mtoto mmoja anaeitwa Gold ambae amezaa na mpenzi wake wa muda mrefu na mwanamuziki mwenzake ambae wameunda kundi linaloitwa NAVY KENZO