Nandy afungukia bifu lake na Ruby

Msanii wa Bongo fleva, Faustina Charles maarufu kama Nandy amesema japo watu wengi wamekuwa wakihoji kuhusu ukaribu wake na msanii wa zamani wa zao la Jumba la kuibua vipaji la THT (Tanzania House of Talent), Ruby kwa madai kuwa kwa sasa hawapikiki chungu kimoja kutokana na ushindani uliopo baina yao, ishu ambayo ameikataa na sio kweli kwani hana bifu na mwanadada huyo.
Kwenye mahojiano aliyofanya hivi karibuni alisema anawashangaa wanavyosema hapatani na Ruby kwa madai kuwa anahukiwa kwa sababu amemfunika mwenzake kimuziki

“Ukiniuliza mimi na Ruby nani anaimba vizuri, nitakujibu wote, yeye ana muziki wake nami nina muziki wangu sina ugomvi wala mazoea naye ila tukikutana tunasalimiana tu kama washkaji”,

download latest music    

Kumekuwa na tetesi mbalimbali za kuwepo kwa bifu kati ya warembo hawa wawili kutokana na ufanano wa muziki wanaofanya japo wamekuwa wakikana kwamba hawana tatizo na ni washkaji tu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.