Nandy Alikuwa Msanii wa WCB Kabla ya Kutoka:Lizer

Mtayatrisha ji wa nyimbo nyingi kutokaWCB Lizer amefunguka na kusema kuwa katika maisha yake elimu yake aliyoishia ni darasa la saba na alifaulu vizuri lakini alikataa shule na kusababisha kufukuzwa nyumbani ndipo alipoamua kukimbilia Burundi alipotokea nyumbani kwao kigoma na ndipo alipoenda kujifunzia muziki.

Lizer anasema kuwa alijifunza kuimba na baadae kuwa producer ndipo moja ya wasanii nchini Burundi alipomtambulisha kwa Diamond lakini Diamond alimuomba kufanya nae kazi na alikataa lakini kutokana na hali ya amani kutokuwa shwari nchini Burundi aliona bora arudi Tanzania ambapo baaada ya muda aliona maisha yanabadilika na kumtafuta Diamond na kukuta nafasi yake bado ipo na ndipo alipoanza kufanya kazi na Diamond.

download latest music    

Hata hivyo alipoendelea kuongea lizer alitoboa siri na kusema kuwa nandy pia alikuwa msani kutoka WCB lakini alipoona amekaa muda mrefu bila kutoa ndipo alipoamua kuanza kufanya kazi zake .

Hata hivyo Lizer anasema kuwa tangu ameanza kufanya kazi na wcb, ndoto zake imewea kutimia kwa 70% na kwamba kuhusu kufanana kwa nyimbo zake katika beats , hiyo ni identity yake ambayo anaitengeneza.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.