“Napenda Wanaume Weusi Nikiwaona Nasisimka”- Linah Sanga

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Ndege Mnana Linah Sanga amefunguka na kuweka wazi kuwa anavutiwa zaidi na wanaume weusi kuliko wanaume  weupe.

Linah alizua gumzo Kwenye social media baada ya kuweka picha ya mpenzi wake na kuweka wazi kuwa anampenda mwanaume wake kwa sababu ni mweuzi sana.

download latest music    

Kwenye Interview na Millard Ayo, Linah amefunguka na kudai anapenda sana wanaume weusi kwani wana muonekano wa kiume zaidi kuliko wanaume weupe.

Mimi hulka yangu napenda wanaume weusi hata ukifatilia Maex wangu asilimia kubwa ni wanaume weusi Barakah The Prince alikuwa mweusi tii tena amezidi hadi baba watoto wangu na hata Amini naye ukimuangalia ni mweusi”.

Lakini pia Linah ameweka wazi kuwa havutiwi kabisa na wanaume weupe:

Sivutiwi kabisa na wanaume weupe yaani nikaona mwanaume mweusi nasisimka ananivutia kwani naona wamekaa kiume zaidi”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.