Nay Wa Mitego na Duma Wameingia Kwenye Bifu Zito

Mwanamuziki wa Bongo fleva Ney Wa Mitego na muigizaji wa Bongo movie Duma wamejikuta wakiwa katika pande mbili tofauti za shilingi baada ya kuingia kwenye bifu zito.

Bifu hili lilianzia kwenye mtandao wa kijamii huko Instagram baada ya Nay Wa Mitego kuweka maoni kwenye picha hiyo kulikuwa kuna wakali watatu wa Bongo movie ambao ni Rammy Gallis, Gabo na Duma na kisha ilisindikizwa na swali liliouliza ‘Je nani  mkali wa fasheni hapo?’ Basi baada ya kuona hivyo Nay Wa Mitego alienda ku-comment na kuandika ‘ Tafadhali msimfananishe Gabo na vitu vya kipuuzi’ maneno ambayo yalimkera sana Duma.

download latest music    

Baada ya maneno hayo kuenea mtandaoni Gabo alimwaga povu lake kwenye mahojiano aliyofanya na kituo cha televisheni cha East Africa;

Kwanza nilikuwa Nairobi nafanya project nikaona hizo comments watu tofauti tofauti wakanitumia mimi nikafurahi nikaona ni kitu kizuri ila naomba nimwambie Bwana Emanuel,  Ney Wa Mitego ameingia choo cha Kasilo kwa sababu ameshawahi kumtibua Niva, alishawahi kumtibua Yusuphu Mlela akatulia tu ila mimi ni namba chafu asione watu wamenyamaza ila mimi peke yake namtosha Ney Wa Mitego yaani mimi ndio namwambia Ney asiingilie mambo ya Bongo movie kama anatafuta kiki akatafute huko huko kwa wanamuziki wenzake asituingilie Bongo movie kwa sababu ameshatuongelea sana mara oh Bongo movie imekufa mara nini sijui sasa basi inatosha namkanya Ney aachane na sisi kama hana ishu arudi kwao Manzese akawe mkabaji maana alijuwa kibaka zamani hivyo awe na heshima maana mwisho wa siku mziki wake umeshuka”.

Pia Duma amedai Ney hana haki ya kuiongelea vibaya Bongo movie kwa sababu pale alipo hana kolabo hata moja na nsanii wa nje lakini hao anaowasema Bongo movie wameigiza na wasanii mbali mbali wa nchi za nje.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.