Nay Wa Mitego: Nliumizwa sana na maneno ya Roma Mkatoliki

Emmanuel Elibariki maarufu kama Nay Wa Mitego amefunguka kuhusu bifu yake na Roma Mkatoliki iliyoonza baada ya Roma kutekwa nyara miezi kadhaa iliyopita.

Roma aliongea maneno ya kumkashifu Nay Wa Mitego mara baada ya yeye kuachiliwa na watu waliomteka nyara akiwa na wenzake kwa studio yake.

download latest music    
Nay Wa Mitego

Nay ata hivyo hana machungu na Roma, rapa huyo alisema yeye bado anamtakia mema Roma hata kama maneno aliyosema juu yake yalimuuma sana.

“Roma anatakiwa ajue kwamba mimi ni mmoja kati ya wasanii ambao walishinda kutwa nzima kwenye studio yake ya Tongwe Records na kituo cha polisi, toka siku aliyotekwa hadi siku aliyopatikana, lengo likiwa ni kutaka kujua tunasaidiana vipi ili aweze kupatikana. Akitaka kuthibitisha hilo amuulize mkewe, lakini nikashangaa baada ya kupatikana eti akanikashifu, kila nikikumbuka inaniumiza, sema mimi ni mwanaume siweki vitu rohoni, na pia nimeipenda sana ngoma yake ya Zimbabwe, Roma ni rapa mkali, sina kipingamizi juu ya hilo,” amesema Nay Wa Mitego.

Roma Mkatoliki

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere