Ney wa Mitego Amchana Diamond Baada ya Kuachwa na Zari

Msanii wa Bongo fleva Ney wa Mitego amemtolea povu zito msanii mwenzake Diamond Platnumz baada ya mpenzi wake Zari kutangaza rasmi kuwa amemuacha kutokana na michepuko kuzidi.

Jana usiku Zari aliwashtua watu wengi baada ya kuweka wazi kuwa ameamua kimya cha Diamond kutokana na kuzidi kudhalilishwa na taarifa za yeye kuwa na michepuko mingi huku mambo yaliyokuwa yanatokea kwenye mitandao ya kijamii yalikuwa yanamuumiza.

download latest music    

Kumekuwa na skendo nyingi mtandaoni za Diamond kuchepuka na wanawake kadhaa huku pia kumekuwa na uthibitisho wa vitendo hivyo lakini kwa muda mrefu Zari alionekana kuvumilia na kumsamehe mpenzi wake huyo lakini safari hii inaelekea maji yalimfika shingoni.

Baada tu ya Zari kutangaza kumwaga Diamond mashabiki walianza kumlaumu Diamond kwa kumuacha mrembo kama Zari aende kwa tabia yake ya kuendekeza michepuko moja kati ya watu hao ni msanii Ney wa Mitego.

Nay kumtolea povu zito Diamond kwa kumuacha mtoto mzuri kama Zari ambaye ana pesa zake na badala yake kuendekeza michepuko ambayo hainam maana ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram Nay wa Mitego alitoa povu hili:

Wanasema chozi la aliyetendwa haliendi bure mwanangu Diamond, Omna sana Mungu akuonyeshe njia la si hivyo utapotea… umempoteza mwanamke ambaye hana njaa ana maisha yake binafsi alichokuwa anataka ni mapenzi yako tu sikatai kuwa hakuna mwanaume asiyekuwa na tamaa lakini ulifeli kufanya uchafu wako wazi wazi”.

Baada ya kutoa povu hili imeonyesha wazi kuwa Nay wa Mitego na Diamond hawana urafiki mzuri kama waliokuwa nao mwanzoni ambapo siku za nyuma kulikuwa kuna habari zikidai kuwa wamekorofishana.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.