“Nibusu Shavuni, Vyovyote Vile, Nakupenda”- Ujumbe Wa Ray C Kwa Ruge

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Rehema Chalamila maarufu kama  Ray C amemtumia ujumbe mzito Mkurugenzi wa Clouds Media Group Ruge Mutahaba.

Ray C ameandika maneno yaliyowashangaza wengi huku yakiwaacha wengine vinywa wazi kwa ujumbe aliomwandikia Ruge  ambaye kwa wakati huu yupo nje ya nchi kwa matibabu.

download latest music    

Kupitia akaunti ya Ray C ya instagram ameandika:

Amka bwana, nashachoka kusubiri, msg zangu hujibu, simu hupokei, na stori kibao nataka kukwambia ingawa najua utanchamba lakini nishazoea kukwambia kila kitu changu kinachoendelea kwenye maisha yangu, tunagombanaga mpaka tunablokiana lakini tukionana tu tukaangaliana tunabaki kucheka tu.

Nishazoea kukwambia mambo yangu sababu we ndo msiri wangu, we ndo unanipaga makavu nikiharibu, Kuna muda mpaka nalia na ukiona nalia ndo unazidi kunipa makavu bila huruma.

Naondoka kwa hasira ingawa moyoni najua uliyoniambia ni kweli…. nakununiaaaaa ila haifiki wiki huyo nishakuja ofisini, Muda mwingine sina hata cha maana cha kukwambia ila nakuja tu ofisini kukuona unitanie nicheke!

Ray C umenimiss eeh…. Kama nywele hujazielewa unanipa live Ray nenda Katoe hizo nywele, Nikikuona tu napata amani ya moyo. Nikitoka tu studio wa kwanza kukutumia demo! ni wewe, wewe tu miaka yote tangu nimeanza muziki sababu naheshimu sikio lako na naliamini.

Mwezi wa ngapi sasa huu Ruge!Natuma msg, nakupigia, natamani kukuimbia japo kidogo upate nguvu sikupati..Ruge najua huko ulipo Unaumia sana,najua unataka kuamka na kufanya kazi zako. PLS WAKE UP babaa. Please!You are too strong babaa, Don’t give up Please..4 U

Nishike mkono, Nibusu shavuni, Vyovyote vile, Nakupenda. (Your favorite song )
#AmkaRuge”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.