Nicole Awaomba Wasanii Wamkomboe Wastara.

Msanii wa bongo movie ambae pia alishawahi kutwaa taji la Miss Shinyanga, Nicole Franklyn amewaomba wasanii wote nchi kuwa na moyo wa kujitolea na kumsaidia msanii mwenzao Wastara Juma ambae anaomba msaada kwa ajili ya kwenda nje kwa ajili ya matibabu yake ya mguu.

Msanii huyo wa bongo movie anaomba wasanii waache kinyongo na kumsaidia msanii mwenzao kwa sababu matatizo yanaweza kumkumba mtu yoyote na hakuna anaeijua kesho yake.nicole anasema kuwa hata kama kuna mtu alishawahi kuwa na kinyongo na Wastara haina haja ya kuangalia makosa bali kusameheana na kusaidia katika matatizo.

download latest music    

ninawasihi na kuwaomba wasanii wenzangu tuungane kumchangia wastara, ili aweze kukamilisha ela yake kwa ajili ya matibabu yake.Ninaamini sapoti ya wasanii aliyopewa bado haitoshi kabisa kwa sababu tukiamka wote atafanikiwa.hata kama kuna mtu anakisasi kwa sasa aweke kando tu  kwa sababu matatizo yanaweza kumfika mtu yoyote.

Wastara amekuwa akiomba msaada kwa muda mrefu ili kukamilisha fedha zinazohitajika kwa matibabu ya mguu wake inayohitaji zaidi ya milioni 30.wastara anatakiwa kurudi nchini india ili aweze kufanyiwa matibab hayo ili kuondokana na maumivu ya mgongo yanayompata kwa kumrudia rudia kila muda.

Hata hivyo bado inasemekana kuwa muamko wa wasanii wenzake na Wastara ni mdogo sana kulingana na hali za wasanii na wingi wao katika tasnia hiyo.Inaaminika kuwa kama wasanii wote wataguswa na tatizo hilo itasaidia kufanikisha na kumsaidia wastara.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.