Nikki wa Pili Awazindua Watanzania kuhusu maktaba mpya ya UDSM

Msanii kutoka katika kundi la Weusi Nikki wa Pili alipata nafasi ya kuzungumzia uzinduzi mpya wa maktaba mpya ya kitaifa iliyojengwa chuo kikuu cha udsm ambapo ilifungukiwa November 27 na Mh rais.

akiandika  kama moja ya watu wanatajwa kuaminika asana kwa mawazo yao kwa vijana , Nikki ukiachana na kuwa msanii lakini pia amekuwa moja ya watu wanaohamasisha sana juu ya maisha na kutia bidii katika kile wanachokifanya na kukiamini.

download latest music    

katika ukurasa wake wa Twitter Nikki wa Pili aliandika “maktaba ya kuchukua wasomaji 2100 ina maana ni fursa kila siku kwa vijana 2100 kujivunia maarifa, itumieni sana itumieni vizuri ili kujenga maarifa vizuri kupanga mawazo na pia kutafuta ukweli wa kile unachoweza kujielezea , hili ni pori adhimu katika maisha, maktaba ni  uhai wa jamii.”

Nikki wa pili anasema kuwa vijana wanatakiwa kujifunza kuitumia maktaba hiyo kwa kujijengea kutafuta habari na maarifa mbalimbali  ili kuwa na wigo mpana wa mawazo.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.