Nikki wa Pili Azungumza na Baraza la Sanaa.

Msanii wa muziki Tanzania Nikki wa Pili amefunguka na kuhoji juu ya vitendo wanavyovifanya baraza la sanaa vya kuwafungua wasanii kama ni vya halali bila kuzingatia mambo mengi na kujikuta wakijikita katika mavazi tu ilhali swala la maadili linakuwa linapande nyingi na sio swala la mavazi tu.

Nikki wa Pili alizungumza hayo alipokuwa naongea na mtangazaji wa EATV na kusema kuwa baraza linatakiwa kuangalia swala la maadili kwa upana sana na sio katika mavazi tu kwa sababu hata kwa upande mwingine ukiangalia utakuta kuwa hata wao kama baraza wanakuwa hawatimizi majukumu yao wa wasanii.

download latest music    

Nikki amesema kuwa Baraza wanakosea wanapokuwa wanawafungia wasanii tena hasa wa kike kwa sabau ya maadili ili hali wanapaswa kuangalia vitu vini kabla ya kutoa uamuzi huo,lakini pia yapo mambo mengi baraza wanatakiwa kuyanyoosha na kuyyaweka katika mstari kabla hawajaanza ku-judge kuhusu mavazi na maadili yao.

Maneno ya nikki yanakuja baada ya Baraza la Sanaa kuwafungia baadhi ya wasanii wa kike kwa madai kuwa wasanii hao wamekuwa wakitoa video na kuchapisha picha za uchi katika mitandao na kutoa ahadi kuwa yeyeto atakae toa wimbo usiokuwa na maadili ya kitanzania basi wimbo huo na kazi zake zitafungiwa.

Wasanii waliofungiwa hivi karibuni kutokana na utovu wa nidhamu katika kazi za muziki ni pamoja na Gigy money na Pretty kindy huku wengine wakiambiwa kuripoti katika ofisi za baraza lakini pia wimbo wa Rostam wa Kibaa100 pia umfungiwa mpaka utakapofanyiwa marekebisho katika baadhi ya vipengele.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.