Niligombana na Mwanangu Kisa Mambo Ya Usanii- Mzee Gerald

Baba mzazi wa marehemu Agnes Gerald ‘Masogange’ Anayeitwa Mzee Gerald amefunguka na kueleza kuwa alikuwa akigombana sana na mwanaye ambaye alikuwa anamsihi aachane na mambo ya sanaa.

Agnes alijizolea umaarufu miaka ya nyuma kwa mara ya kwanza baada ya kutokea kwenye video ya wimbo wa Msanii wa Bongo fleva Belle 9 Masogange ambao ulipelekea mpaka yeye kuitwa Agnes Masogange Lakini pia marehemu alikuwa ameanza kuwa muigizaji wa Bongo movie.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers kwa mara ya kwanza tangu amzike mwanaye hapo jana, Mzee Gerald amefunguka haya kuhusu binti yake:

Mwanangu alikomea kidato cha pili lakini hata kidato  cha pili hakumaliza kwa sababu ya matatizo. Kuna wakati nilikorofishana naye nikamwambia mimi mambo ya usanii sitaki, akanijibu, ‘sasa baba mimi nitafanya kazi gani wakati unafahamu tangu niko kanisani nilikuwa naimba kwaya?’ Baada ya muda tulikutana tena, tukalimaliza suala hilo, nikamruhusu“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.