“Nilikutana na Diamond Club Miaka Miwili Iliyopita”- Tanasha

Mtangazaji na video vixen maarufu kutoka nchini Kenya Tanasha Donna Oketh ambaye pia ni Mpenzi wa  staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz amefunguka na kuweka wazi Jinsi walivyokutana.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Tanasha aliwapa mashabiki zake uhuru wa kumuuliza maswali ambapo alifunguka kwa Kuwapa majibu.

download latest music    

Tanasha aliulizwa ni Jinsi gani alikutana na Mpenzi Wake Diamond na aliweka wazi kuwa walikutana miaka miwili iliyopita walipokuwa Club Lakini hawakuwahi kuongea Mpaka mwaka jana mwishoni.

Nilikutana naye miaka miwili iliyopita klabu Lakini hatukuwahi kuongea mpaka mwaka jana mwishoni”.

Lakini pia Tanasha alianika mapenzi yake kwa Diamond na kusema wazi wazi kuwa anampenda sana Diamond na pia kusema ana sifa zote za mwanaume ambaye angependa kuwa naye yaani ni muaminifu, mchapakazi, ana Upendo na sifa nyingine kedekede.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.