“Nilipata Matatizo Mimba Yangu Ikaharibika”-Shamsa Ford

Muigizaji wa Bongo movie Shamsa Ford amefunguka mazito kuhusu jitihada zake za kushika mimba ambapo amesema alishika ujauzito mwaka jana lakini kwa bahati mbaya mimba ikatoka.

Shamsa amefunguka na kuelezea janga hilo lililomkuta miezi michache iliyopita ambapo alidai kutoka na matatizo aliyoyapata mume wake Chidi ambaye aliwekwa rumande kwa tuhuma za kuuza na kuingiza nchini madawa ya kulevya.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Lemutuz Online Shamsa Ford amefunguka zaidi haya:

Mimi naamini watoto wanaletwa na Mwenyezi Mungu kwa bahati mbaya au bahati nzuri nilishika ujauzito kipindi kile mume wangu kapata matatizo yale ya kuwekwa ndani na mimi mimba yangu ikatoka naona ilikuwa hofu ndio maana, unajua hapa mjini mume wangu hana ndugu kwaiyo mimi ndio nilikuwa kila kitu yaani nihahakikishe biashara zinaenda vizuri muda huo huo nikamuangalie Mume wangu ana hali gani kule polisi kwaiyo nilikuwa very stressed kwaiyo nikajikuta mwisho wa siku mimba yangu ya wiki tatu ikatoka”.

Shamsa ameolewa na Chiddi Mapenzi ambaye ni mfanyabiashara maarufu Lakini tangu wanafunga ndoa yao mwaka jana maneno mengi sana yalisemwa juu ya Mahusiano yao ikiwemo wapo waliodai hawatodumu jambo ambalo Shamsa amesema halitakuja litokee kwani wapo wote mpaka kifo kitakapowatenganisha.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.