“Nina Mpango Wa Kuirudisha TMK Wanaume”- Mh. Temba

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva nchini Amani Temba maarufu kama Mh. Temba amefunguka na kuweka wazi mipango yake ya kuirudisha Kundi lao la Wanaume TMK.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Mh. Temba amesema Kundi la TMK Wanaume litarudi na kuanza kazi ya muziki kama lilivyokuwa zamani ili Kuthibitisha hilo, Temba alisema anatarajia kuandaa kolabo moja matata mwaka huu wa 2019 ili kurudisha rasmi kundi hilo.

download latest music    

Nitawalea wimbo ambao utakuwa na vichwa vyote vya TMK Wanaume niliousimamia mimi, nataka kukata kiu ya mashabiki waliokuwa wanatamani kutuona pamoja”.

Lakini pia Temba alisema wanatarajia ujio wao huo kuwa wa tofauti kwa kubadilisha mfumo wa utendaji wa kazi kutoka wimbo kuwa na dakika tano na kuwa dakika tatu.

Kundi la TMK Wanaume lililokuwa na wasanii wakongwe kama Chege, Temba, Juma nature na wengineo lilivunjika miaka ya nyuma Baada ya mgogoro mkubwa kuhusu uongozi na maslahi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.