Nina Ndoto Ya Kumvalisha Rihanna Kwenye Video Zake-Wolper

Muigizaji wa Bongo movie na mwanamitindo Jacqueline Wolper ambaye amekuwa akishona nguo zake kama fundi cherehani amefunguka na kudai anataka kumvisha staa wa kimataifa Rihanna.

Wolper amevaa cha watu midomo wazi baada ya kusema Yupo katika harakati za kumtafuta Mwanamuziki wa kimataifa kutoka Marekani Rihanna ili aweze kumshonea nguo ili aweze kuvaa.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Waandishi wa habari katika red carpet ya event ya Jibebe Challenge Wolper alifunguka:

 Kwa sasa bado naendelea kusoma nikimaliza nadhani nitaendelea na preocess za kumtafuta Rihanna kwa ajili ya kumvalisha na shukurani kwa mitandao ya kijamii ambayo imenipa wepesi wa kumtafuta Rihanna”.

Wolper ameswashangaa wanaodai haitawezekana kwake yeye kuwavalisha mastaa wakubwa kama Rihanna na kusema kila kitu kinawezekana ni kuweka juhudi Kwenye kazi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.