Nuh Mziwanda (ex wake Shilole): Sitaki mambo ya wanawake yaani staki hata kusikia

Nuh Mziwanda bado ako na uchungu tangu aachane na mke wake anayefahamika kwa jina la Nawal. Msanii huyo sasa anawachukia wanameke kwa dhati.

Akiongea katika kipindi cha 5seleKt kutoka EATV, Nuh Mziwanda alisema yeye sasa ni single boy baada ya kuachana na mke wake siku chache zilizopita.

download latest music    
Nuh Mziwanda

Nuh aliwahi kuwa na mahusiano na mwanamuziki Shilole kabla ya kuachana naye na kumoa mkewe Nawal ambaye alimzalia mtoto mmoja.

Nuh sasa amesema hataki mambo ya wanawake tena, alifunguka na kusema kuwa anatamani kukaa na mtoto wake ambaye kwa sasa anaichi na mkewe tangu waachane.

Nuh Mziwanda na mkewe

“Sasa hivi nipo ‘single boy’ sitaki mambo ya wanawake yaani staki hata kusikia. Nilitamani sana mtoto wangu ning’ekaa naye mimi ‘since’ yupo mdogo lakini nashindwa kufanya hivyo kwa sababu ya umri wake haujifikia kukaa na baba kwa hiyo nimemuachia mama yake kwa sasa lakini kama nikiona mwanangu wanamfanyia vitu ambavyo si sawa kwangu nitaenda kumchukua nikae naye mimi mwenyewe,” Nuh Mziwanda alisema.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere