Odemba Akubali Kuporwa Mume
Mwanadada ambae amekuwa katika mitindo kwa muda mrefu Miriam Odemba anekiri kuachana na mume wake kwa muda sasa baada ya bwana huyo kushindwa kukaa nae kutokana na u-bize wa kazi anazofanya za uana mitindo , hivyo kujikuta akishawishika kujiingiza katika mahusiano na mwanamke mwingine aliyekuwa akimpatia muda mwingi.
Habari za hapo awali za chii chini zilikuwa zikisema kuwa mwanadada huyo kwa sasa amekuwa akiishi peke yake na kulea mtoto mwenyewe huko mume wake akimwachia majukumu hayo.
Habari kutoka kwa watu wa karibu wa Odemba walipotoa taarfa hizo,GPL waliamua kumtafuta miriam mwenyewe na kukiri kuwa kwa sasa nyumbani kwake anakaa pekee yake na mtoto.
Anasema ” okay ngoja niweke wazi kwa sababu naona mmeshapata habari, unajua mimi mara nyingi nimekuwa mtu wa kusafiri safiri kutokana na kazi zangu, kwaio baada ya kusafiri mwenzangu akapata vishawishi na kwa sababu mwenzangu ana jina kubwa sana huku kwaio nikaona bora mimi nikae pembeni tu. ‘Hata msichana mwenyewe pia ninamjua naomba ifahamike kuwa mimi na yeye ni mtu na mzazi mwenzie tu na hatukuwahi kufunga ndoa.