Ommy Dimpoz atii onyo kali kutoka kwa dadake Diamond Platnumz

Diamond Platnumz, Alikiba na Ommy Dimpoz wamekua wakitupiana maneno yenye mafumbo katika mitandao ya kijamii tangu Diamond aliposhirikishwa katika remix ya ngoma ya Fid Q ‘Fresh’.

Bifu hio baina ya wasanii hao watatu ilifanya Ommy Dimpoz kuweka picha Instagram akiwa na mama mzazi wa Diamond na kuandika ujumbe wenye utata.

download latest music    

Aunty Ezekiel ambaye ni meneja wa zamani wa Ommy Dimpoz na dadake Diamond walitoa onyo kali kwa Ommy Dimpoz kukoma kumuingiza mamake Diamond katika ugomvi wake na Diamond.

Onyo hilo kutoka kwa dadake Diamond na mashabiki kadhaa ilichangia Ommy Dimpoz kuamua kuifuta post yake ya utata aliyoiweka kwenye Instagram.

Account ya Ommy Dimpoz ya Instagram ikionyesha kuwa alitoa post ya utata akiwa na mamake Diamond

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere