Ommy Hatoimba Tena , Hilo Najua :-Steve nyerere.
Msanii wa vichekesho nchini, Steve Nyerere amefunguka na kusema kuwa anavyojua kuhusu hali ya ommy dimpoz mwanamuziki huyo hawezi kuimba tena kwa sababu hana sauti kama aliyokuwa nayo hapo mwanzo.
steve anasema kuwa tangu hapo awali yeye alikuwa mtu wa kwanza kujua hali ya Ommy lakini hata aliposema hadharani wapo waliomuona kama anataka kiki hivyo waliamua kumbeza lakini yeye alikuwa akijua ukweli.
Ommy ni mwanamuziki na mungu amembariki namimi ndio mtu wa kwanza kumposti na kusema ommy pole sana kwa maradhi hayo, wengune wakanibeza lakini nilikuwa najua nini kinaendelea.tunachotakiwa kufanya, najua ommy hatoimba tena kwa sababu ili uimbe inabidi uwe na vocal
Ikumbukwe kuwa Ommy dimpoz alifanyiwa uapasuaji wa koo kutokana na atahari alizopata baada ya kuonekana kuwa alikunywa kinywaji chenye sumu kilichoharibu mfumo wake wa koo na kusababisha kushindwa kumeza vitu.