Penzi la Linah na Mumewe Ladaiwa Kulega Baada ya Kuzaa

Msanii wa Bongo fleva Linah Sanga amerudi tena kwenye vichwa vya habari huku safari hii sababu ikiwa ni mapenzi, ambapo inadaiwa penzi la Linah na mpenzi wake limeingia shubiri kidogo tangu azae.

Linah ana uhusiano wa kimapenzi na Shaban Mchomvu ambaye ni maarufu kama Director Ghost ambaye amezaa naye mtoto mmoja wa kike anayeitwa Tracey Paris.

download latest music    

Lakini tetesi zilizosambaa chini chini ni kwamba inadaiwa mapenzi yamepungua kati ya Linah na mumewe tangu ajifungue mtoto wao mwaka jana lakini pia inadaiwa Director ghost anajitahidi kumpa kila kitu mpenzi wake Linah ikiwa ni pamoja na kutengeneza studio ndani ya nyumba yao ili Linah asitoke nje ya nyumba.

Kwenye interview na ENews ya East Africa Tv, Linah amefungukia tetesi hizi na pia inadaiwa penzi limeisha kwani amekuwa hamposti Tena mumewe kama zamani:

Kwanza nitamposti niijisikia unajua kile kitu unatakiwa ufanye kwa kujisikia sio usukumwe na watu eti kisa unaogopa watu watafikiria mmeachana sababu mimi na yeye sahivi tuna miaka miwili na kitu kwenye mahusiano tumeshajuana tushakuwa tayari kama mume na mke kwaiyo kuna vitu vingine tunaona ni utoto tu havina faida labda tuseme nimempunguzia kasi lakini sio kwamba ndio simpendi au nini ila yeye ni mtu simple na ana mambo yake binafsi hana muda wa kufanya mambo ya kitoto”.

Linah amekana tetesi za yeye kuwa na ugomvi na mumewe na kusema wanafanya mambo yao private lakini pia amekiri kuwa hapendi kumposti sana kwani anavyojigamba naye sana kuna nyaku nyaku wanapata wivu na kuna wasichana wengine watataka kutembea na bwana wa mtu ilimradi wamkomeshe mke wake sababu ya kuringa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.