Penzi Langu na Shamsa Ford Halina Dalili Ya Kuvunjika- Chidi Mapenzi

Mfanyabiashara maarufu Kwenye mitandao ya kijamii Rashid maarufu kama Chidi Mapenzi ambaye pia ni mume wa msanii wa Bongo movie Shamsa Ford ameweka wazi kuwa hana Mpango wa kuachana na mke wake.

Chidi Mapenzi amekanusha tetesi zinazodai  kwamba penzi lao lipo hatarini kuvunjika huku akidai kwa sasa wapo vizuri na wanafurahia maisha yao.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Kipindi cha Shilawadu cha Clouds Tv,  Chidi amedai kuwa siri ya kudumu kwao ni kutambua kosa lake na kuamua kujishusha mara moja:

Mimi ni mke wangu huwa hatugombani, nikimkwaza lazima niwe chini nitafanyaje Mke wangu nikimkosea huwa anakuwa na hasira lakini baadaye hasira zinaisha na maisha yanaendelea”.

Chidi amesema sio kweli kwamba ndoa yao ilikuwa ivunjike, yote ambayo yalikuwa yanazungumzwa na mitandao ya kijamii kwamba ndoa yao ipo mbioni kuvunjika sio ya kweli.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.